CHUKUA HIZI FORMULA...

 



HILI SOMO LITAKUWEZESHA KUTENGENEZA CHAKULA CHA MIFUGO WAKO KIURAHISI HAPO NYUMBANI KWAKO.

katika somo la leo tutangalia namna ya kuweza kuchanganya vyakula vya mifugo mbali mbili pia kulingana na uhitaji wao, tambua kua zoezi la kuchanganya vyakula ni muhimu sana kwako wewe mfugaji kwani kufanya hivo utapunguza gharama za kununua vyakula madukani, hapa kinacho hitajika kwanza nielimu ya uchangaji wa vyakula vya mifugo, jabmbo jema hiyo elimu unaipata hapa kupita makala hii ya lugalo animal care, kitu kingine cha kuwa nacho ni marighafi,

✓ hakikisha chakula utakacho kipata baada ya mchanganyiko kina viini vifuatavyo

1. protini 

2. wanga

3. madini

4 mafuta 

5 na maji

MWISHO WA SOMO HILI UTAWEZA KUTENGENEZA CHAKULA CHA MAKUNDI YA WAVYAMA WAFUATAO

vifaranga nyama anza/broiler starter, vifaranga nyama kuzia, vifaranga mayai kuzia, chick mash, kuku mayai kuzia, kuku mayai taga, nguruwe watoto, nguruwe nenepesha, nguruwe kuzia, na ng'ombe wa maziwa,

Tuanzie hapa:

VIFARANGA VYAMA AZA

pumba 76kg

mashudu alizeti 15kg

dagaa sagwa 7kg

chokaa mifugo 0.5kg

premix 0.5kg

chumvi sagwa 0.5kg

VIFARANGA MAYAI ANZA

pumba 78kg

mashudu alizeti 16kg

dagaa sagwa 5kg

chokaa mifugo 2kg

premix 0.5kgkg

chumvi sagwa 0.5kg 

NGURUWE WATOTO 

pumba 76kg

mashudu alizeti 15kg

dagaa sagwa 6kg

chokaa mifugo 2kg

premix 0.5kg

chumvi sagwa 0.5kg

NGURUWE WA KUKUZA

pumba 76kg

mashudu alizeti 15kg

dagaa sagwa 4kg

premix 0.5kg

chumvi sagwa 0.5kg

NGURUWE NENEPESHA

pumba 80kg

mashudu alizeti 15kg

dagaa sagwa 2kg

chumvi sagwa 0.5kg

premix 0.5kg

KUKU MAYAI KUZIA

pumba 80kg

mashudu alizeti 12kg

dagaa sagwa 5kg

chokaa mifugo 2kg

premix 0.5kg

chumvi 0.5kg

KUKU MAYAI TAGA

pumba 80kg

mashudu alizeti 14kg

dagaa sagwa 3kg

chokaa mifugo 2kg

premix 0.5kg

chumvi sagwa 0.5kg

Kumbuka premix zina unzwa kwenye maduka ya bidhaa za mifugo, kwahiyo kama ulivyoona hapo juu kuwa premix imehusika katika kila mchanganyiko, na premix zipo za aina nyingi, mfano kama wewe unataka kutengeneza chakula cha kuku waliopo kwenye hatua ya kukua ( growers ) basi utanunua growers premix, kama ni kuku wanyama basi utanunua broiler premix, hivyo hivyo na kwenye Makundi mengine

pia sehemu yenye pumba unaweza gawanya mchanganyiko kwa mfano kama pumba inahitajika 80kg basi utachukua 20kg za mahindi palaza na 20kg za pumba pia kwenye chokaa utachukua nusu ya chokaa na nusu 

na mifupa sagwa kwenye jumla ya kilo za choka zinazohitajika katka huo mchanganyiko.


Post a Comment

Previous Post Next Post